Monday, 9 June 2025

Wazee 2 hadi 3 kati ya 10 hufanyiwa ukatili Bunda

 

Afisa ustawi wa jamii halmashauri ya mji wa Bunda mkoani Mara Waryoba Juma

Baadhi ya wazee wameitaka serikali iwatambue wazee kwamba wapo, pia iwahudumie hasa katika sera ya matibabu bure kwa wazee maana wakati mwingine hukosa dawa kwenye vituo vya kutolea huduma za afya

Na Adelinus Banenwa

Imeelezwa kuwa wazee wawili (2)hadi watatu (3) kati ya wazee kumi (10) halmashauri ya mji wa Bunda hufanyiwa ukatili mbalimbali katika jamii na familia.

Hayo yamesemwa leo na afisa ustawi wa jamii halmashauri ya mji wa Bunda mkoani Mara Waryoba Juma ambapo amesema takwimu hizo siyo nzuri lakini pia siyo mbaya ukilinganisha na maeneo mengine nchini.

Waryoba amesema ukatili wanaokutana nao wazee ni pamoja na kubaguliwa, kunyanyaswa, kutosikilizwa na wakati mwingine wazee wanapigwa  matukio ambayo matukio haya yanagawanyika katika makundi mawili ya unyanyasaji ambayo ni kimwili na kisaikolojia.

Waryoba ameyasema hayo katika kikao kilichowakutanisha wazee kutoka mitaa ya kata ya Sazira walipokuta na viongozi wa baraza la ushauri la wazee halmashauri ya mji wa Bunda.

Sauti ya Waryoba Juma

Kwa upande wao baadhi ya wazee wameitaka serikali iwatambue wazee na kwamba wapo pia iwahudumie hasa katika sera ya matibabu bure kwa wazee maana wakati mwingine hukosa dawa kwenye vituo vya kutolea huduma za afya pia watoto wao kushindwa kuwalea na badala yake huwarundikia wajukuu nyumbani bila utaratibu.

Baadhi ya wazee waliohudhulia kikao cha wazee Sazira
Sauti ya baadhi ya wazee

Naye Machael Kweka ambaye ni mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Bunda na diwani wa kata ya Sazira  ameiomba serikali  kuleta mpango wa kulipa pensheni kwa wazee wa Tanzania bara kama inavyofanyika huko Zanzibar na lingine watoto wenye kazi kuhakikisha wanawakatia bima za matibabu wazee wao.

Sauti ya Michael Kweka

Sunday, 8 June 2025

Auawa na tembo akilinda shamba la Nyanya Bunda

 

Alikuwa analinda mazao yake yasiliwe na tembo na ndiyo kawaida yetu maana bila kulinda huwezi kuvuna chochote.

Na Adelinus Banenwa

Kijana mmoja aliyetambulika kwa jina la Kinyunyi Nyakile mkazi wa mtaa wa Ichamu kata ya Kunzugu Halmashauri ya mji wa Bunda mkoani Mara amepteza maisha baada ya kushambuliwa na tembo wakati akilinda bustani yake ya nyanya.

Tukio hilo linatajwa kutokea usiku wa kuamkia Juni 8, 2025 ambapo inaelezwa kundi la tembo zaidi ya watano walifika karibu na mashamba ya wakulima hapo Kunzugu ndipo wakulima walianza kuwafukuza lakini tembo mmoja aligeuka na kuanza kuwakimbiza hadi alipomshika Kinyunyi na kumkanyaga vibaya hali iliyopelekea kupoteza maisha.

Mwenyekiti wa mtaa wa Ichamu James Magwayega Haruna ameiambia mazingira fm kuwa tukio hilo limewasikitisha kutokana na kupoteza nguvu kazi ya mtaa na imekuwa kawaida kwa wakazi wa mtaa wake ili wavune mazao yao ya shambani ni lazima kulinda.

Sauti ya Mwenyekiti wa mtaa wa Ichamu James Magwayega Haruna

Kwa upande wake Magambo Magambo ambaye ni baba mdogo wa marehemu Kinyunyi amesema kama familia wamepoteza mtu muhimu sana hasa ukizingatia alikuwa bado mdogo na alikuwa hajawa na familia Aidha ameiomba serikali kujenga uzio kuzuia wanyama hao ili kunusuru maisha ya wananchi na mazao.

Sauti ya Magambo Magambo ambaye ni baba mdogo wa marehemu

Naye diwani wa kata ya Kunzugu Mhe Pasaka Samson amesema taarifa za mwananchi wake alizipata usiku ambapo alichukua hatua ya kwenda hadi eneo la tukio kisha aliwasiliana na mamlaka mbalimbali ikiwemo watu wa Kikosi dhidi ya ujangiri KDU, Jeshi la polisi pamoja na ofisi ya mkuu wa wilaya.

Mhe Pasaka amesisitiza kuwa serikali ione umuhimu wa kuongeza gari la doria kwa kuwa lililopo halitoshi kuanzia Balili hadi Tungirima ambao ni ukanda wote wa hifadhi ya taifa ya Serengeti.

Sauti ya diwani wa kata ya Kunzugu Mhe Pasaka Samson

Friday, 6 June 2025

Wafugaji kufanya kongamano kubwa June, 15 na 16

 

Mwenyekiti wa Chama cha Wafugaji Tanzania, Ndugu Mrida Mshota

Watu zaidi ya laki moja wakitalajiwa kuudhulia katika kongamano hilo

Na Thomas Masalu

Chama cha Wafugaji Tanzania kimetangaza kufanyika kwa kongamano maalum la siku mbili litakalofanyika tarehe 15 na 16 Juni mwaka huu, katika viwanja vya nane nane , Nyakabindi mkoani Simiyu huku watu zaidi ya laki moja wakitalajiwa kuudhulia katika kongamano hilo linalolenga uzinduzi wa chanjo ya mifugo na utambuzi pamoja na kujadili changamoto na fursa zilizopo katika sekta ya ufugaji nchini.

Akizungumza na Redio Mazingira FM, leo tarehe 6/6/2025 kupitia kipindi cha Duru za Habari, Mwenyekiti wa Chama cha Wafugaji Tanzania, Ndugu Mrida Mshota, amesema kuwa maandalizi ya kongamano hilo yanaendelea vizuri.

Aidha mwenyekiti huyo wa chama cha wafugaji Tanzania Mrida Mshota ameeleza kuwa Mgeni Rasmi katika Kongamano hilo maaalum la siku mbili, anatarajiwa kuwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Daktari Samia Suluhu Hassan,

Sauti ya Mwenyekiti wa Chama cha Wafugaji Tanzania, Ndugu Mrida Mshota

Huku akiongeza kuwa kongamano hilo linalotarajiwa kuwahusisha wafugaji kutoka mikoa mbalimbali nchini, huku likitarajia kutoa afua ya masuala ya sera za ufugaji, teknolojia mpya, masoko ya bidhaa za mifugo, pamoja na umuhimu wa uhifadhi wa mazingira katika shughuli za ufugaji.

kwa Kuwa ni mara ya ya kwanza kwa Tanzania kuwa na kongamano la kitaifa la utoaji chanjo na utambuzi kwa mifugo jambo ambalo limefanyika katika uongozi wa awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan.

Sauti ya Mwenyekiti wa Chama cha Wafugaji Tanzania, Ndugu Mrida Mshota

Wednesday, 4 June 2025

Vikundi vya ulinzi shirikishi hupunguza uhalifu kwenye jamii

 

Mkaguzi wa polisi Jonas Kaijage ambaye ni mratibu wa polisi jamii wilayani Bunda

Bunda kuna jumla ya vikundi 31 vya ulinzi shirikishi ambavyo vipo hai na katika maeneo hayo matukio ya uharifu yamepungua kwa kiasi kikubwa.

Na Adelinus Banenwa

Imeelezwa kuwa sehemu zenye vikundi vya ulinzi shirikishi yaani polisi jamii wilayani Bunda matukio ya kiharifu yamepungua kwa kiasi kikubwa ukilinganisha na maeneo ambayo hakuna kabisa vikundi hivyo.

Hayo yamesemwa na mkaguzi wa polisi Jonas Kaijage ambaye ni mratibu wa polisi jamii wilayani Bunda kupitia kipindi cha Asubuhi leo kinachorushwa Radio Mazingira fm ambapo amesema kwa wilaya ya Bunda kuna jumla ya vikundi 31 vya ulinzi shirikishi ambavyo vipo hai na katika maeneo hayo matukio ya uharifu yamepungua kwa kiasi kikubwa.

Kaijage ameongeza kuwa sheria ya kuwepo kwa ulinzi shirikishi una lengo la kuishirikisha jamii katika masuala ya ulinzi na usalama katika maeneo yao ndiyo maana kama jeshi la polisi wanahusika kutoa elimu na maelekezo kwa vikundi vinavyoanzishwa.

Kaijage ametoa wito kwa jamii kuhakikisha kupitia kwa wenyeviti wa mitaa, vijiji na vitongoji wanaanzisha vikundi hivyo ili kuweka usalama kwenye maeneo yao kwa kuwa sasa jeshi la polisi limesogeza karibu kabisa huduma na vikundi hivyo ikiwa nipamoja na kila kata kuwepo kwa polisi kata ambaye anasaidia kutoa elimu kwa vikundi hivyo.

Sauti ya Jonas Kaijage ambaye ni mratibu wa polisi jamii wilayani Bunda

Kwa upande mwingine Insp Kaijage amewataka wafanyabiashara wanaotoa huduma za kifedha kwa maana ya huduma pesa kuwa waangalifu kutokana na changamoto za wizi na utapeli ambao unaonekana kushamili kwa siku za hivi karibuni.

Sauti ya Jonas Kaijage ambaye ni mratibu wa polisi jamii wilayani Bunda

Thursday, 29 May 2025

Wananchi wahimizwa kutunza na kuwahifadhi kobe

 

Lusato Masinde Afisa wanyamapori kutoka TAWA kanda ya ziwa ,picha na Catherine Msafiri

Kobe ni wanyama kama walivyo wanyamapori wengine na wanalindwa kisheria tuwatunze.

Na Catherine Msafiri,

Jamii imetakiwa kuendelea kuwatunza na kuwalinda kobe kwaajiri ya manufaa ya vizazi vijavyo kwani ujangili dhidi yao unahatarisha uwepo wa mnyama kobe kwa miaka ijayo.

Hayo yameelezwa na afisa wanyamapori kutoka TAWA kanda ya ziwa ndugu,Lusato Masinde alipofanya mahojiano na radio Mazingira fm kwenye kipindi cha uhifadhi na utalii.

Afisa wanyamapori TAWA kanda ya ziwa Lusato Masinde

Aidha Masinde ameeleza kuwa binadamu ndie kiumbe hatari zaidi kwa mnyama kobe kutokana na shughuli zao hasa pindi wanapochoma misitu
Pia amebainisha kuwa mnyama kobe anafaida mbalimbali kiuchumi, kiikolojia na kijamii

Sauti ya Afisa wanyamapori kutoka TAWA kanda ziwa Lusato Masinde

Hata hivyo ameeleza sifa za mnyama kobe huku akibainisha kuwa kisheria watu wanaweza kuanzisha mashamba ya kufuga kobe isipokuwa tu kwa kuzingatia sheria na taratibu.

Sauti ya Afisa wanyamapori kutoka TAWA kanda ziwa Lusato Masinde

Friday, 16 May 2025

wanafunzi Migungani Sekondari watembelea Mazingira fm

 




Baadhi ya wanafunzi wa kidato cha nne kutoka Shule ya Sekondari Migungani wakiwa kwenye chumba cha kurushia matangazo radio Mazingira Fm

Wamesema kuwa ziara hiyo imewapanua uelewa wao kuhusu namna vyombo vya habari vinavyofanya kazi.

Na Taro Michael

Wanafunzi wa kidato cha nne kutoka Shule ya Sekondari Migungani, iliyopo wilayani Bunda, mkoani Mara, wamefanya ziara ya kielimu katika Redio Mazingira FM kwa lengo la kujifunza kwa vitendo kuhusu mawasiliano na utangazaji wa redio.

Ziara hiyo ni sehemu ya mtaala wa elimu unaolenga kuwajengea wanafunzi uelewa wa kina kupitia mafunzo ya vitendo, hasa katika masomo ya lugha, uraia, na teknolojia ya habari na mawasiliano (TEHAMA).

Baadhi ya wanafunzi wa kidato cha nne kutoka Shule ya Sekondari Migungani wakiwa nje ya ofiza za radio Mazingira Fm

Wanafunzi hao takribani 20 walipata fursa ya kutembelea vitengo mbalimbali vya utangazaji, kujionea kwa macho namna vipindi vinavyoandaliwa, kurekodiwa na hatimaye kurushwa hewani. Pia walijifunza mbinu za ukusanyaji wa habari, uandishi wa taarifa na uhariri wa vipindi vya redio.

Aidha baadhi ya wanafunzi walieleza kufurahishwa na kile walichojifunza. Wamesema kuwa ziara hiyo imewapanua uelewa wao kuhusu namna vyombo vya habari vinavyofanya kazi na kuwaongezea ari ya kuchangia maendeleo kupitia fani ya mawasiliano.

sauti za wanafunzi

Thursday, 8 May 2025

Aswege: Halmashauri toeni elimu ya mikopo kwa wanawake wajasiriamali

 

Mkuu wa wilaya ya Bunda  Mhe Aswege Enock Kaminyoge

Tangu kuanzishwa kwa jukwaa hili mwaka 2005 limesaidia wanawake wengi katika kuhakikisha wanazifikia ndoto zao

Na Adelinus Banenwa

Mkuu wa wilaya ya Bunda  Mhe Aswege Enock Kaminyoge amezielekeza halmashauri za wilaya ya Bunda kuandaa program maalumu kwa ajili ya kutoa elimu ya mikopo kwa akina mama wajasiriamali ambao wanajiunga katika vikundi ili kupunguza changamoto za mikopo kwa akina mama hao

Dc kaminyoke ametoa maelekezo hay oleo may 8 2025 katika uzinduzi wa chemba ya wanawake wajasiriamali wilaya ya Bunda chini ya TANZANIA WOMEN CHEMBER OF COMARCE.

Sauti ya Mhe Aswege Enock Kaminyoge
Baadhi ya wanachama na wanufaika wa chemba TWCC

Baadhi ya wanachama na wanufaika wa chemba hiyo wamesema kuna fursa mbalimbali kwa wanawake kujiunga na umoja huo kutokana na kukutanishwa na wataalamu mbalimbali pamoja na taasisi za serikali zinazowapatia elimu ili kukabiliana na changamoto za kibiashara katika ujasiriamali wao

Aidha wametoa wito kwa wanawake wengine kutoogopa kujiunga na jukwaa hili kwa kuwa wapo walioanza pasipo kuwa na uelewa lakini hadi hivi sasa wametengeneza mtandao mkubwa wa biashara.

sauti ya wanufaika wa jukwaa la TWCC
Baadhi ya wajasiriamali waliojiungq na jukwaa la TWCC wakionesha walivyoongeza thamani Bidhaa zao

Kwa upande wake mkurugenzi wa jukwaa hili la TWCC Maria Isidory amesema tangu kuanzishwa kwa jukwaa hili mwaka 2005 limesaidia wanawake wengi katika kuhakikisha wanazifikia ndoto zao katika kuwasaidia elimu ya biashara, mitaji na kuwakutanisha na wataalamu pamoja na taasisi za serikali kama vile  TRA, SIDO miongoni mwa taasisi zingine

Sauti ya mkurugenzi wa jukwaa hili la TWCC Maria Isidory

Upatikanaji wa samaki wengi waathiri biashara ya nyama Bunda

 

Wateja wamepungua kwa kasi katika siku za hivi karibuni kutokana na watu wengi kuelekeza nguvu zao katika kununua samaki

Na Thomas Masalu

Imeelezwa kuwa katika mji wa Bunda, upatikanaji mkubwa wa samaki kwa sasa umeanza kuathiri kwa kiasi kikubwa biashara ya nyama ya ng’ombe, hali inayowatia hofu baadhi ya wafanyabiashara wa nyama hiyo.

Wafanyabiashara hao wamesema kuwa wateja wamepungua kwa kasi katika siku za hivi karibuni kutokana na watu wengi kuelekeza nguvu zao katika kununua samaki ambao wanapatikana kwa wingi sokoni.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti leo Mei 7, 2025, na redio Mazingira FM katika eneo la genge la jioni, wafanyabiashara hao wameeleza kuwa tofauti ya bei kati ya samaki na nyama ya ng’ombe imechangia kushuka kwa mzunguko wa biashara yao.

Wafanyabiashara hao wamesema kuwa licha ya changamoto hiyo, bado wana matumaini kuwa hali itabadilika pindi upatikanaji wa samaki utakapopungua.

Sauti ya Wafanyabiashara

Tuesday, 6 May 2025

Waliolipwa Nyatwali watakiwa kuondoka

 

Mkuu wa mkoa wa Mara Kanal Evance Mtambi

Serikali tayari imetoa bilioni 53 kwa ajili ya ulipaji wa fidia kwa wakazi hao ili kuachia maeneo hayo yawe sehemu ya hifadhi ya taifa ya Serengeti.

Na Adelinus Banenwa

Wananchi wa Nyatwali ambao tayari wamelipwa stahiki zao kwa utaratibu wa kisheria watakiwa kuondoka.

Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa mkoa wa Mara Kanal Evance Mtambi katika kilele cha maadhimisho ya siku ya urithi wa dunia na afrika yaliyofanyika wilayani Serengeti mkoani Mara leo tarehe 5 May 2025.

Kanal Mtambi amesema serikali tayari imetoa bilioni 53 kwa ajili ya ulipaji wa fidia kwa wakazi hao ili kuachia maeneo hayo yawe sehemu ya hifadhi ya taifa ya Serengeti.

Baadhi ya wananchi waliohudhuria maadhimisho ya siku ya urithi duniani

Kanal Mtambi amesema eneo la Nyatwali tangu enzi za ukoloni lilionekana si sehemu salama kwa makazi ya binadamu na wakati huo lilitambulika kama guba ya speek na utaratibu wa wananchi waliokuwa eneo hilo kuhamishwa ulianza muda mrefu lakini serikali ya awamu ya sita imefanikisha jambo hilo.

Aidha mkuu wa mkoa wa Mara amesema kiasi cha malipo kilichosalia kinaendelea kulipwa kwa utaratibu uliowekwa

Sauti ya mkuu wa mkoa wa Mara Kanal Evance Mtambi

Friday, 2 May 2025

Amuua mpenzi wake kisha na yeye kujinyonga; Bunda

 

Ndege Makebe Karando (31) amuua kwa kumchoma visu aliyekuwa mpenzi wake ambaye ni muhudumu wa afya katika zahanati ya marambeka Zawadi John Kazi (35) kisha na yeye kujinyonga.

Na Adelinu Banenwa

Vilio na sintofahamu vimeendelea kutawala kwa wakazi wa kijiji cha Marambeka kata ya Ketare halmashauri ya wilaya ya Bunda kufuatia tukio la Ndege Makebe Karando (31) kumuua kwa kumchoma visu aliyekuwa mpenzi wake ambaye ni muhudumu wa afya katika zahanati ya marambeka Zawadi John Kazi (35) kisha na yeye kujinyonga.

Makebe Karando baba mzazi wa ndege amesema tukio hilo la kijana wake kufanya mauaji kisha na yeye kujinyonga limewaachia majonzi makubwa kutokana na wote waliopoteza maisha alikuwa akiwachukulia kama watoto wake.

Mama mzazi wa Ndege Makebe

Makebe amesema karando alikuwa na wake wawili lakini pia alikuwa na mahusiano na muhudumu huyo wa afya na tayari walishajitambulisha kwake na mara ya mwisho ilipotokea sintofahamu baina yao walimfikia na akawashauli na walimuhakikishia kuwa mgogoro umeisha hadi pale alipopata taarifa za tukio la mtoto wake Ndege kumshambulia Zawadi

Makebe anaeleza kuwa majira ya usiku alipokea taarifa za Zawadi kushambuliwa na Ndege lakini alikuwa hajamuona ndege japo taarifa za ujio wake pale kijijini alikuwa nazo kwa kuwa mtoto wake huyo anaishi maeneo ya Mugumu Serengeti ambako ana mke mwingine

Familia ya Ndege Makebe wakiwa msibani

Ameongeza kuwa wakati asubuhi kesho yake wanajiandaa kama nzengo kujikusanya ili waanze kumtafuta ndege na kumtia nguvuni kutokana na tukio alilolifanya ndipo alipopata taarifa kuwa mtoto wake huyo amekutwa shambani akiwa amejinyonga kwenye mti aina ya mkwaju na alpokwenda alishuhudia kweli Ndege amejinyonga

Makebe Karando

Ngei Mashoka rafiki wa karibu wa ndege ameiambia Mazingira fm kuwa aligundua kuwa rafiki yake amejinyonga baada ya kupigiwa simu kutoka Musoma kutoka kwa rafiki yao mwingine akidai amepokea simu kutoka kwa Ndege akidai anaenda kujiua kwa kujinyonga katika moja ya miti iliyo shambani mwake

Ngei Mashoka rafiki yake Ndege na liyegundua kuwa Ndege amejinyonga

Huku rafiki huyo akieleza kuwa maelekezo ya ndege yalikuwa endapo watamkuta ameshakufa wamtumie nauli mke wake aliyeko Mugumu aje kwenye msiba

Ngei Mashoka

Hata hivyo baadhi ya viongozi katika kijiji hicho akiwemo diwani wa kata ya Ketare Mramba Simba Nyamkinda na mwenyekiti wa kijiji Ramadhani Lukiko wamekemea tabia za vijana kujichukulia sheria mkononi huku wakitoa wito kuwa endapo kuna sintofahamu kwa watu wenye mahusiano ni vema wakapata suluhu kutoka kwa viongozi

viongozi diwani na mwenyekiti

Jeshi la polisi kupitia kwa kamanda wa polisi mkoa wa Para Pius Lutumo limethibitisha kutokea kwa matukio hayo mawili yaani kuuawa kwa Zawadi John na Ndege Makebe kujinyonga kwenye mti kwa kutumia shuka huku chanzo cha tukio hilo kikitajwa kuwa ni wivu wa kimapenzi baada ya marehemu Zawadi kukataa kuendelea kuwa na mahusiano na Ndege.

Zawadi John Kazi aliyekuwa muhudumu wa afya katika zahanati ya Marambeka inatajwa ameacha watoto wawili huku Ndege Makebe akitajwa kuacha wajane wawili na watoto watano