Baraza la madiwani Bunda TC wapitisha bajeti ya bilion 2.24 ya TARURA kwa 2025 na 2026
27 February 2025,

Fedha hizo zikipitishwa kama zilivyopendekezwa zitakwenda kutelezeza hatua tofauti za ujenzi wa miundombinu ya barabara kama vile ujenzi wa barabara mpya, ujenzi wa mitaro, uwekaji wa taa za barabarani maeneo ya senta pamoja na ujenzi wa madaraja na karuvati.
Na Adelinus Banenwa
Baraza la madiwani la halmshauri ya mji wa Bunda limepitisha shilingi Bilion 2.24 kama makadirio ya bajeti ya TARURA kwa mwaka wa fedha 2025 na 2026 ili kutekeleza hatua mbalimbali za ujenzi wa miundombinu ya barabara kwa halmashauri ya mji wa Bunda.
Akiwasilisha mapendekezo hayo meneja wa wakala wa barabara za mijini na vijijini TARURA muhandisi Ahimidiwe Kiruswa mbele ya baraza hilo la madiwani amesema katika fedha hizo zikipitishwa kama zilivyopendekezwa zitakwenda kutelezeza hatua tofauti za ujenzi wa miundombinu ya barabara kama vile ujenzi wa barabara mpya, ujenzi wa mitaro, uwekaji wa taa za barabarani maeneo ya senta pamoja na ujenzi wa madaraja na karuvati.

Katika ushauri wao baadhi ya madiwani wa halmashauri hiyo wamemtaka meneja huyo wa TARURA kuhakikisha anamaliza viporo vya barabara vilivyobaki katika mwaka wa fedha 2023 na 2024 pia kuamalizia mpango wa utekelezaji wa mwaka 2024 na 2025.
Aidha madiwani hao wamemtaka meneja huyo wa TARURA kuhakikisha anawasimamia wakandarasi wanaopewa kazi za ujenzi wa miundombinu ya barabara kutokana na wakandarasi hao kuwa na tabia ya kutelekeza kazi na kuacha changamoto kubwa kwa wananchi,

Naye katibu tawala wilaya ya Bunda ndugu Salumu Mtelela amempongeza meneja wa TARURA kwa kuendelea kusimamia uboreshaji wa miundombinu ya barabara mjini Bunda huku akimuelekeza kuendelea kusikiliza ushauri unaotoka kwa madiwani kwa kuwa hao ndiyo wanaoishi katika maeneo yao na changamoto kubwa za barabara wanafahamu zipo maeneo gani.
No comments:
Post a Comment