- Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Thursday, 20 February 2025

 

NHIF yaja na vifurushi vipya kuongeza wigo wa matibabu kwa wateja

20 February 2025, 

Afisa Wanachama Mwandamizi NHIF mkoa wa Mara, Felister Renatus,(picha na Edward Lucas)

Jamii yatakiwa kuwa na utamaduni wa kukata bima ya afya kabla ya kuugua ili kuepuka changamoto mbalimbali za kupata huduma

By Edward Lucas,

NHIF yaja na kifurushi cha NGORONGORO AFYA na SERENGETI AFYA ili kuongeza wigo wa matibabu kwa wateja na kutoa punguzo la asilimia 10 ya mchango wa wategemezi kwa kujiunga na familia

Akizungumzia mpango huo kupitia Radio Mazingira Fm, Afisa Wanachama Mwandamizi NHIF mkoa wa Mara, Felister Renatus amesema kwa vifurushi vilivyokuwepo awali vilikuwa na kikomo cha matibabu lakini kwa vifurushi hivi vipya vimeongeza wigo zaidi wa matibabu nchi nzima katika vituo vya matibabu zaidi ya elfu 10 walivyovisajili kwa ngazi ya zahanati hadi taifa

Sauti ya Felister Renatus, Afisa Wanachama Mwandamizi NHIF mkoa wa Mara

Akitoa mfano wa huduma zilizoongezwa katika vifurushi vipya ni pamoja na huduma za kuchuja damu, huduma za saratani, kuboresha zaidi huduma za upasuaji mkubwa na mdogo, maboresho ya huduma za vipimo kama CT Scan na MRI pamoja na huduma za uzazi

Felister Renatus, Afisa NHIF Mara akitaja huduma
Felister Renatus, Afisa Wanachama Mwandamizi NHIF mkoa wa Mara (picha na Edward Lucas)

Aidha Bi, Felister amesema NHIF imezindua na kurejesha huduma ya Toto Afya Kadi ambayo ilizuiliwa kwa muda ili kufanya maboresho ambapo baada ya maboresho huduma hiyo imerejea rasmi hivyo amewaasa wazazi kukata huduma hiyo kwa ajili ya watoto wao

Felister Renatus

Kwa upande wake Mhasibu Mwandamizi NHIF Mkoa wa Mara, Vistus Tilusasila ameiasa jamii kuwa na utamaduni wa kukata bima ya afya kabla ya kuugua ili kuepuka changamoto mbalimbali za kupata huduma

Vistus Tilusasila, Mhasibu Mwandamizi NHIF mkoa wa Mara (Picha na Elia Martine)
Vistus Tilusasila

No comments:

Post a Comment