- Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Saturday, 22 February 2025

 

Pamba yavaliwa njuga Bunda, matarajio makubwa ya uzalishaji

22 February 2025,

katibu tawala wilaya ya Bunda Salumu Mtelela

Imeelezwa kuwa Serikali kupitia bodi ya pamba Tanzania imedhamilia wakulima wa zao hilo kulima kwa tija badala ya kulima mashamba makubwa lakini mavuno kidogo.

Hayo yamesemwa na mkaguzi wa zao la pamba wilayani Bunda Ndugu Hemedi Kabea mbele ya katibu tawala wa wilaya hiyo Ndugu Salumu Mtelela wakati wa ziara ya kukagua maendeleo ya kilimo cha zao la pamba wilayani Bunda na kujionea hali ya huduma zinazotolewa na bodi ya pamba kwa wakulima wa zao hilo.

Mkaguzi wa zao la pamba wilayani Bunda Ndugu Hemedi Kabea

Kabea amesema jitihada mbalimbali zimefanywa na serikali kupitia bodi ya pamba ili kuongeza tija katika uzalishaji wa zao hilo ambapo serikali imeleta mbegu za kutosha, dawa kwa maana ya viuadudu, vinyunyizi, matrekta, pamoja na Droni.

Sauti ya mkaguzi wa zao la pamba wilayani Bunda Ndugu Hemedi Kabea

Naye katibu tawala wilaya ya Bunda Salumu Mtelela ameishukuru bodi ya pamba kwa kuendelea kusimamia zao la pamba ambalo ni miongoni mazao mkakati kwa wilaya ya Bunda

Katibu tawala akizungumza na wananchi katika maeneo ya mashamba amesema wilaya ya Bunda kwa msimu huu wa kilimo inatakiwa kuzalisha tani elfu 20 sawa anasilimia 67% ya pamba yote inayotakiwa kuzalishwa katika mkoa wote wa Mara hali hiyo inaifanya wilaya ya Bunda kuwa wilaya kinara katika uzalishaji wa zao la Pamba kimkoa.

katibu tawala wilaya ya Bunda Salumu Mtelela

Mtelela amewapongeza wataalamu wa kilimo kwa kuendelea kubuni njia mbalimbali za kudhibiti wadudu kwenye mashamba zikiwemo njia za asili kama vile matumiszi ya mimea ya alizeti pamoja na tenolojia ya morasisi lakini amesema serikali pia imeleta droni tano wilayani Bunda ambazo zitasaidia katika kunyunyiza dawa kwenye mashamba ya wakulima kwa haraka na kwa muda mfupi

Mtelela ameendelea kuwarai viongozi wote pamoja na wananchi kujiepusha na hujuma zozote zile zinazosababisha hasara kwa serikali na zao lenyewe ikiwemo wizi wa viuadudu pamoja na uzembe katika kupulizia viuatilifu kwenye mashamba.

Sauti ya katibu tawala wilaya ya Bunda Salumu Mtelela
Baadhi ya viongozi na wananchi katika ziara ya pamba Bunda

Kwa upande wao wakulima wameipongeza serikali kwa kuendelea kuweka mkazo katika zao la pamba hasa katika usimamizi lakini wameitaka serikali kuwaletea viuadudu kwa wakati pia wametaja changamoto ya Mabadiliko ya tabia ya nchi kama kikwazo ikiwemo mvua kubwa na wakati mwingine ukame .

No comments:

Post a Comment