- Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Thursday, 6 March 2025

 

Anusurika kifo baada ya kushambuliwa na mamba akioga

6 March 2025, 5:29 pm

Anusurika kifo baada ya kushambuliwa na Mamba alipokwenda ziwani asubuhi, rafiki apanda juu ya mamba kunusuru ndugu yake.

Na Adelinus Banenwa

Kijana mmoja aliyetambulika kwa jina la Baraka Jumanne Maseke mwanafunzi wa kidato cha nne shule ya sekondari Neruma kata ya Neruma halmashauri ya wilaya ya Bunda amenusurika kifo baada ya kushambuliwa na Mamba alipokwenda ziwani asubuhi.

Akizungumza na Mazingira fm mjomba wa kijana huyo aitwaye Exavely Palapala amesema tukio hilo limetokea asubuhi ya tarehe 5 March 2025 majira ya saa kumi na mbili asubuhi ambapo Baraka akiwa ameambatana na rafiki yake aitwaye Dotto Maingu Elias walikwenda ziwani kuoga ili kwenda shule.

Palapala ameongeza kuwa kwa mujibu wa maelezo yao baada kufika ziwani Baraka alikuwa wa kwanza kuingia kwenye maji ndipo alipo dakwa na mamba muda mfupi tu baada ya kuanza kuoga.

Sauti ya Exavely Palapala Mjomba wa Baraka,

Kwa upande wake Dotto Maingu aliyekuwa ameambatana na Baraka ameiambia Mazingira fm kuwa baada tu ya kufika ziwani Baraka alitangulia kuingia majini na yeye alibaki akiwa amekaa ufukweni.

Anasema baada ya muda mfupi tu alisikia kelele za rafiki yake akiwa kwenye maji akiomba msaada ndipo alipovua ngua haraka na kujitosa kwenye maji ili aone namna ya kumsaidia.

Sauti ya Dotto Maingu rafiki yake Baraka

Naye mwenyekiti wa kikiji cha Kasaunga ndugu Benard James Nyamwega amesema ni kweli taarifa za tukio hilo anazo na kuwa tukio hilo lilitokea jana lakini vijana hao hawakwenda kuoga bali kuangali mitego yao ya samaki ndipo mmojawapo akashambuliwa na mamba.

Sauti ya mwenyekiti wa kikiji cha Kasaunga ndugu Benard James Nyamwega

Baraka kwa sasa a anapatiwa matibabu katika Hospitali ya mkoa ya mwal Nyerere ya mkoani maarufu hospitali ya Kwangwa.

No comments:

Post a Comment