Mbunge Ghati ahimiza ushirikiano kwa wanawake

Mbali na kuwataka wanawake kuwa na mshikamano pia amesema ni lazima zisemwe kazi nzuri zilizofanywa na serikali awamu ya sita chini ya rais Samia Suluhu Hassan
Na Adelinus Banenwa
Wito umetolewa kwa wanawake wote kuwa na ushirikiano na kujenga tabia ya kupendana ili kutimiza adhma ya nafasi ya mwanamke katika jamii.
Hayo yamesemwa leo tarehe 7 March 2025 na mbunge viti maalumu mkoa wa Mara kupitia kundi la wanawake Mhe Ghati Chomete katika maadhimisho ya siku ya wanawake duniani ambapo kwa wilaya ya Bunda yamefanyika leo katika viwanja vya CCM wilaya ya Bunda.

Mbunge Chomete kama mgeni rasmi katika maadhimisho hayo wilayani Bunda mbali na kuwataka wanawake kuwa na mshikamano pia amesema ni lazima zisemwe kazi nzuri zilizofanywa na serikali awamu ya sita chini ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kama vile miundombinu ya maji barabara, umeme elimu miongoni mwa kazi zingine.

Naye mwenyekiti wa CCM wilaya ya Bunda Ndugu Abraham Mayaya Magese amewapongeza wanawake kwa kuadhimisha siku yao huku akisema chama cha mapinduzi kinatambua mchango mkubwa unafanywa na wanawake viongozi wa chama cha mapinduzi na serikali huku akiwata viongozi hao kutatua kero za wananchi kila mmoja kwa eneo alilopo iwe ni ngazi ya mtaa au kijiji, Kata, mpaka wilaya.
Aidha viongozi hao wasemema kazi kubwa ya CCM ni kuangalia na kutatua kero za wananchi wakitolea mfano utatuzi wa migogoro baada ya tamko la hivi karibuni kuhusu mabasi kusitisha kushusha abiria katika vituo vya Nyasura na Bunda DDH ambapo kupitia viongozi hao wameeleza kuwa tayari malalamiko ya bodaboda na wajasiliamali yamefanyiwa kazi na mabasi yataendelea kushusha abiria katika vituo hivyo.
Miongoni mwa viongozi waliokuwepo kwenye Maadhimisho hayo ya siku ya wanawake Duniani ni pamoja na Mwenyekiti wa kamati ya fedha, mipango na uchumi chama cha mapinduzi wilaya ya Bunda Eng Kambarage Masatu Wasira ambaye amesema kuna kila sababu ya kuwapongeza wanawake kwa hatua kubwa ya kimaendeleo walizopiga
Kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake duniani hufanyika March 8, ambapo kwa mwaka huu kitaifa yanatarajiwa kufanyika mkoani Arusha ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan
No comments:
Post a Comment