- Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Tuesday, 4 March 2025

 

Mtoto Angel aliyezama kwenye rambo apatikana akiwa amefariki

4 March 2025, 

Kaimu kamanda wa zimamoto na uokoaji mkoa wa Mara Agostino Magere

Mwili wa mtoto huyo umeopolewa na askari wa zimamoto na uokoaji walikuwa eneo la tukio tangu March 2, 2025 walipopata taarifa za tukio hilo.

Na Adelinus Banenwa

Mtoto Angel Wilson 8 mwanafunzi wa darasa la pili shule ya msingi Kataryo B halmashauri ya Musoma Vijijini mkoani Mara aliyedaiwa kuzama kwenye bwana la maji amepatikana akiwa amefariki.

Kaimu kamanda wa zimamoto na uokoaji mkoa wa Mara Agostino Magere amesema mwili wa mtoto huyo umeopolewa leo na askari wa zimamoto na uokoaji walikuwa eneo la tukio tangu March 2, 2025 walipopata taarifa za tukio hilo.

Magere amesema chanzo cha tukio hilo ni kukosekana kwa umakini ambapo mtoto Angel Wilson akiwa na dada yake wa kidato cha tatu walikwenda kuchota maji ambapo maeneo hayo ni hatari kwa usalama hali iliyopelekea mtoto huyo kutereza na kuzama.

Sauti ya Kaimu kamanda wa zimamoto na uokoaji mkoa wa Mara Agostino Magere

Magere ametoa rai kwa wananchi kujenga tabia ya kulitaarifu jeshi la zimamoto na uokoaji mkoa wa Mara mapema pindi kunapohitajika maokozi ama ya moto au watu kuzama majini.

No comments:

Post a Comment