- Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Monday, 3 March 2025

 

Mtoto wa miaka 8 azama maji kwenye rambo wakati akichota maji

3 March 2025, 

Angel Wilson ( 8) mwanafunzi wa darasa la pili shule ya msingi Kataryo B halmashauri ya Musoma Vijijini anatajwa kuzama kwenye rambo wakati akiteka maji.

Na Adelinus Banenwa

Mtoto mmoja aliyetambulika kwa jina la Angel Wilson ( 8) mwanafunzi wa darasa la pili shule ya msingi Kataryo B halmashauri ya Musoma Vijijini mkoani Mara anatajwa kuzama kwenye rambo wakati akiteka maji.

Akizungumza na Mazingira fm baba mzazi wa mtoto huyo Wilson Wilson amesema alipata taarifa za mtoto wake kudumbikia kwenye mashimo hayo ambayo ni mabaki sehemu yaliyokuwa machimbo ya dhahabu.

Wilson amesema alifanya jitihada za kuwasiliana na viongozi akiwemo afisa madini, jeshi la polisi pamoja na jeshi la zimamoto na uokoaji.

Amesema changamoto kubwa katika eneo hilo ni kwamba mashimo hayo ambayo yalikuwa machimbo ambyo kwa sasa yamejaa maji yapo kwenye makazi ya watu lichaya kuwa kuna walinzi lakini wananchi huenda pale na kuchota maji na kunywesha mifugo.

Sauti ya baba mzazi wa mtoto huyo Wilson Wilson

Kaimu kaimu kamanda wa zimamoto na uokoaji mkoa wa Mara Agostino Magere amesema taarifa za mtoto huyo kuzama kwenye bwana hilo walizipata siku ya tarehe 2 March na baada ya kufika eneo la tukio taratibu za maokozi zilianza na kutokana na changamoto ya giza pamoja kina kirefu walilazimika kusitisha zoezi mpaka March 3, 2025.

Sauti ya Kaimu kaimu kamanda wa zimamoto na uokoaji mkoa wa Mara Agostino Magere

Aidha kamanda Magere ametoa wito kwa wananchi hasa wazazi na walezi kuhakikisha wanawachunga watoto hasa katika maeneo hatarishi kama visimani, kwenye madimbwi , au kuchezea vitu vya moto.

No comments:

Post a Comment