Nyamuswa yetu kwanza yadhamiria kurudisha tabasamu kijijini
3 March 2025,

Kikundi hicho kilianzishwa tangu mwaka 2021 na kilianza katika dhima ya kusaidia watu misibani na kusaidia batibabu kwa wale wanaougua lakini hawana uwezo wa kwenda hospitali.
Na Adelinus Banenwa
Kiasi cha pesa taslimu shilingi milioni moja laki sita na elfu therathini na ahadi shilingi milioni nane Mifuko ya saruji 338 pamoja na mabati 108 vimepatikana kwenye harambee ya kuboresha miundombinu ya shule ya msingi Nyansirori.

Harambee hiyo imeandaliwa na kikundi cha vijana cha Nyamuswa Yetu kwanza ambacho kinapatikana katika kitongoji cha Nyamuswa, kijiji cha Mekomariro, kata ya Mihingo halmashauri ya wilaya ya Bunda.

Akizungumza katika harambee hiyo Mikinyemi Sepeku kwa niaba ya katibu tawala mkoa wa Mara ambaye alikuwa mgeni rasmi amesema shule hiyo ni miongoni mwa shule ambazo zinahitaji maboresho makubwa kutokana na miundombinu yake kuchakaa Amewapongeza kikundi kilichoandaa harambee hiyo ili kusaidia kuboresha shule hiyo.
Kwa upande wake mwalimu Jafari ambaye ni miongoni mwa walimu kutoka shule ya msingi Nyansirori akisoma taarifa ya shule amebainisha changamoto mbalimbali ambazo zinaikabili shule hiyo kuwa ni pamoja na upungufu wa madarasa, nyoo, madawati, nyumba za walimu miongoni mwa mahitaji mengine.
Naye mwenyekiti wa kikundi cha Nyamuswa yetu kwanza ndugu Innocent Joseph amesema kikundi hicho kilianzishwa tangu mwaka 2021 na kilianza katika dhima ya kusaidia watu misibani na kusaidia batibabu kwa wale wanaougua lakini hawana uwezo wa kwenda hospitali.
Innocent ameongeza kuwa baadaye kikundi hicho kiliona ni vema pia kikajikita kwenye maendeleo hivyo wameamua kuanza na shule ya msingi Nyansirori ambapo hadi sasa wameshajichangisha kiasi cha shilingi milioni 13.4 na leo wameamua kuhitisha harambee ili wadau waweze kuwaunga mkono.
Katika harambee hiyo baadhi ya viongozi waliochangia kwa ahadi ni pamoja na ofisi ya mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Bunda kwa kushirikiana na ofisi ya mbunge wa jimbo la Bunda kutoa bati 108, mbunge wa jimbo la Bunda ameahidi kujenga madarasa mawili kwa thamani ya milioni 50 na mtatiro Nyamuhanga Kitinkwi pamoja na marafiki zake wakiahidi kutoa shilingi milioni 6
No comments:
Post a Comment