- Mazingira FM

Mazingira Fm Live

Breaking News

Sunday, 2 March 2025

 

Onyo wafanyabiashara watakaopandisha bei bidhaa za chakula Ramadhani na kwaresma

2 March 2025, 

Katibu tawala wilaya ya Bunda Ndugu Salumu Mtelela

Mara nyingi malalamiko ya wananchi yamekuwa ni kwenye bidhaa za mihogo, viazi, tambi sukari miongoni mwa bidhaa zingine.

Na Adelinus Banenwa

Wafanyabiashara wilayani Bunda wametakiwa kujiepusha na upandishaji holela wa bei ya bidhaa za chakula katika kipindi hiki cha mwezi wa Ramadhani na kwaresma.

Akizungumza na radio mazingira fm ofisini kwake katibu tawala wilaya ya Bunda Ndugu Salumu Mtelela amesema serikali inafuatilia kwa ukaribu sana mwenendo wa bidhaa kulingana na bei ya soko ilivyo.

Amesema mara nyingi malalamiko ya wananchi yamekuwa ni kwenye bidhaa za mihogo, viazi, tambi sukari miongoni mwa bidhaa zingine hivyo amewataka wafanyabiashara mbali na kufuata sheria pia wanatakiwa kuwa na utu kwa kuwa kipindi cha mfungo ni ibada.

Mtelela amesema mtu yeyote atakayepata taarifa za mfanyabiashara yeyote anapandisha bei ya bidhaa za chakula katika kipindi hiki bila kufuata utaratibu atoe taarifa kwa wenyeviti au watendaji au ofisi ya mkuu wa wilaya naserikali haitasita kumchulia hatua mtu yeyote atakayekiuka sheria.

Sauti ya katibu tawala wilaya ya Bunda Ndugu Salumu Mtelela

No comments:

Post a Comment